kuongeza
hatari ya kupata saratani hata
zikitumiwa
kwa kiasi kidogo tu. Nyama
hizi
zinahusishwa na saratani za kinywa,
koo,
tezi la kiume (prostate), utumbo
mpana
na mapafu. Inashauriwa kuepuka kutumia
nyama zilizosindikwa. Nyama hizo
ni pamoja na zile zilizosindikwa au
kuhifadhiwa kwa chumvi, mafuta,kemikali
au kukaushwa kwa moshi. Mfano wa nyama hizo ni soseji, nyama za kopo,
hot-dog, salami, bacon.
Umuhimu wa mazoezi ya mwili.
Mazoezi
ya mwili ni muhimu kwa binadamu wote, awe mtoto au
mtu
mzima, mnene au mwembamba, mgonjwa au mwenye afya njema. Mazoezi
hupunguza
uwezekano wa kupata saratani, ugonjwa wa kisukari, ugonjwa wa moyo,
na shinikizo kubwa la damu. Mazoezi ya mwili pia husaidia kudhibiti
magojwa
hayo. Umuhimu mwingine wa mazoezi ya mwili ni kupunguza maumivu ya
tumbo yanayotokea wakati wa hedhi, kuzuia ongezeko la uzito wa mwili,kupunguza
msongo wa mawazo na pia huboresha afya ya akili ikiwa ni pamoja na
kuboresha uwezo wa kufikiri, kuelewa (cognitive ability) na kukumbuka.
Kiwango kiitajiwacho kwa mazoezi ya mwili.
Ili
kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa sugu
yasiyoambukizwa,
fanya mazoezi ya mwili angalau kwa dakika
30
kila siku. Yaani, dakika 30 za mazoezi yanayotumia
nguvu
kiasi kama kutembea kwa haraka (brisk walk).
Unapoanza
unaweza kutembea muda mfupi, na baada ya
kuzoea
unaweza kuongeza muda hadi dakika 60 kwa siku,
na
ukishindwa kabisa kufanya kila siku, fanya angalau
dakika
60 mara tatu kwa wiki.
Namna
ya kuongeza mazoezi:
•
Kama unatumia gari, panga shughuli ambazo
utafanya
kila siku kwa kutembea kwa miguu.
•
Endapo unaishi au kufanya kazi ghorofani jitahidi na
jizoeshe
kutumia ngazi kila siku badala ya lifti.
•
Unapoenda mahali kwa kutembea tumia njia ndefu badala
ya njia ya
mkato.
•
Punguza muda unaotumia kutazama televisheni na utumie
muda huo
kufanya
shughuli zinazotumia viungo vya mwili kama kufua, kuosha
vyombo,
kuosha gari, kusafisha nyumba, kazi za bustani, kufyeka majani.
•
Ongeza matumizi ya redio, kwani mara nyingi unaweza
kufanya shughuli
mbalimbali
huku ukisikiliza redio na ikiwezekana uwe na redio ndogo
ambayo
unaweza kuihamisha na kuiweka mahali unapofanya shughuli
zako
au mazoezi ya mwili.
•
Watoto wawe na muda wa kucheza kila siku, michezo
ambayo inatumia
viungo
vya mwili kama kukimbia, kucheza mpira, kuruka kamba nk.
Kumbuka,
kila zoezi la mwili unalofanya hata kama ni kidogo sio sawa na
kutofanya
kabisa, ni afadhali ufanye kwa kiasi chochote unachoweza kila siku,
halafu
uongeze polepole.
No comments:
Post a Comment
wasiliana nami