ulaji
bora:
•
Kula mlo kamili mara tatu kwa siku. Hii hukuwezesha kupata
virutubishi
muhimu vinavyohitajika mwilini. Mlo kamili hutokana
na
kuchanganya angalau chakula kimoja kutoka katika kila kundi la
vyakula
na viliwe kwa kiasi cha kutosha. Makundi hayo ya vyakula
ni
:
-
Vyakula vya nafaka, mizizi na ndizi. Mfano: vyakula vya nafaka
ni
mahindi, ngano, mchele, ulezi, mtama na uwele; mizizi - viazi
vitamu,
viazi mviringo, magimbi, viazi vikuu, mihogo; ndizindizi
zote
za kupika.
-
Vyakula vya jamii ya kunde na vya asili ya
wanyama. Mfano: vyakula vya jamii
ya kundemaharagwe,
kunde,
njugu mawe, mbaazi, njegere,
choroko,
karanga, dengu na fiwi. Vyakula vya asili
ya wanyama- nyama aina zote, samaki,
maziwa,
jibini,
dagaa, mayai na wadudu wanaoliwa (kama
kumbikumbi,
senene na nzige).
-
Mbogamboga. Mbogamboga zinajumuisha zile za majani
yanayoliwa
(kama majani ya maboga, kunde, matembele,
mchicha,
sukuma-wiki, spinachi, kisamvu, mchunga,
figili,
mnafu, mlenda), na mbogamboga nyingine kama
karoti,
bamia, nyanya, biringanya, maboga, matango,
nyanya
chungu na mamung’unya.
-
Matunda. Mfano mapera, mabungo, ubuyu, ukwaju,
mananasi,
maembe, machungwa, mafenesi, mastafeli,
machenza,
zambarau, matopetope, mapesheni, mapapai, mikoche,
maembe
ng’ong’o n.k.
-
Mafuta na sukari. Mfano: Mafuta; siagi, mafuta ya kupikia mbegu
zitoazo
mafuta (kama ufuta, korosho, kweme, karanga n.k) na sukari
(kama
sukari nyeupe na sukari guru) .
•
Kula matunda na mbogamboga kwa wingi kila siku. Mbogamboga
na
matunda husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini, hivyo
kujikinga
na maradhi mbalimbali. Vyakula hivi pia huupatia mwili
makapi-mlo
ambayo humfanya mtu ajisikie kushiba na kufanya mtu
ale
kwa kiasi, hivyo kupunguza uwezekano wa kuwa na uzito uliozidi
au
unene.
•
Ongeza ulaji wa vyakula vyenye makapi-mlo kwa wingi. Makapimlo
husaidia
mfumo wa chakula kufanya kazi kwa ufanisi. Pia
humsaidia
mtu kupata haja kubwa kwa urahisi na huchangia katika
kupunguza
uwezekano wa kuongezeka uzito, kupata baadhi ya
saratani,
magonjwa ya moyo na kisukari. Unaweza kuongeza kiasi
cha
makapi-mlo kwa kula matunda na mbogamboga kwa wingi,
nafaka
zisizokobolewa kama unga wa dona na ngano (kama atta) na
vyakula
vya jamii ya kunde.
•
Epuka vyakula vyenye mafuta mengi. Mafuta ni muhimu mwilini
lakini
yanahitajika kwa kiasi kidogo. Mafuta huongeza uzito kwa
haraka.
Ulaji wa mafuta mengi huweza kuleta madhara mwilini kama
vile
unene, kuongeza uwezekano wa kupata maradhi sugu kama
magonjwa
ya moyo, kisukari na shinikizo kubwa la damu. Unaweza
kupunguza
kiasi cha mafuta kwa kubadili njia za mapishi, kama
kuoka,
kuchemsha au kuchoma badala ya kukaanga. Pia kuchagua
nyama
isiyo na mafuta na kuepuka asusa zenye mafuta mengi.
•
Epuka kutumia sukari nyingi. Sukari huongeza nishati-lishe mwilini
na
hivyo kuchangia ongezeko la uzito wa mwili ambao huweza
kusababisha
mtu kupata maradhi sugu yasiyoambukizwa. Matumizi
ya
sukari huweza kupunguzwa kwa kunywa vinywaji visivyo na
sukari
nyingi, kunywa juisi halisi ya matunda (isiyoongezwa sukari),
kuepuka
vyakula vyenye sukari nyingi kama soda, juisi bandia, jamu,
biskuti,
keki, chokoleti, kashata na pipi.
•
Epuka kula vyakula vyenye chumvi nyingi.
Ulaji
wa vyakula vyenye chumvi nyingi huongeza
uwezekano
wa kupata shinikizo kubwa la damu
na
baadhi ya saratani. Matumizi ya chumvi nyingi
huweza
kupunguzwa kwa kutumia chumvi kidogo
wakati
wa kupika, kuepuka vyakula vyenye chumvi
nyingi
au vilivyosindikwa kwa chumvi. Pia jenga
tabia
ya kutoongeza chumvi kwenye chakula wakati
wa
kula.
•
Kunywa maji safi, salama na ya kutosha
Kunywa
maji angalau glasi nane (lita moja na nusu) kwa siku. Maji
ni
muhimu sana mwilini kwani hurekebisha joto la mwili, husaidia
katika
uyeyushwaji wa chakula, husafirisha virutubishi kwenda
kwenye
seli na huondoa mabaki au uchafu mwilini kwa njia ya jasho,
mkojo
n.k. Vilevile maji husaidia kulainisha maungio ya mwili.
•
Kula asusa zilizobora kilishe. Kuwa mwerevu na muelewa kwa
kuchagua
asusa zenye virutubishi vingi na muhimu kama matunda,
maziwa,
juisi halisi ya matunda, karanga au korosho. Asusa zitumike
kwa
kiasi. Epuka asusa zenye mafuta mengi (kama sambusa, soseji
kababu,
chipsi), pia zenye sukari nyingi (kama chokoleti, keki,
pipi,
kashata) au zenye chumvi nyingi (kama krispi, soseji) kwani
huweza
kusababisha ongezeko kubwa la uzito na uwezekano wa
kupata
magonjwa sugu yasiyoambukizwa kama kisukari, saratani,
shinikizo
kubwa la damu na maradhi ya moyo. Chagua vyakula
vilivyochemshwa,
vilivyookwa au kuchomwa kama ndizi, mihogo,
mahindi
na viazi.
No comments:
Post a Comment
wasiliana nami