Thursday, 11 September 2014

Faida za asali kiafya


Asali hutumika sio tu kama chakula bali baadhi ya watu huitumia
pia kama dawa. Asali ina uwezo wa kuondoa chembe chembe
haribifu mwilini na hivyo kuulinda mwili dhidi ya maradhi mbalimbali. Asali
ina virutubishi mbalimbali ikiwa ni pamoja na vitamini, madini na protini kwa
kiasi kidogo. Vilevile, asali ina sukari nyingi ambayo ni asilimia themanini (80%).
Kutokana na asali kuwa na sukari nyingi, asali ina nishati-lishe nyingi kama ilivyo
sukari, hivyo ikitumika kwa wingi huongeza uzito wa mwili.
Asali iliyokomaa kwa kawaida ina kiasi kidogo cha maji, chini ya asilimia ishirini
(20%). Asali iliyoongezewa maji inachacha mapema (inaharibika) na inaota
ukungu (fangasi), ambao wakati mwingine hauonekani kwa macho. Kwa kawaida
asali iliyokomaa na isiyochanganywa maji ikihifadhiwa vizuri haiharibiki kwa
miaka mingi, bila hata ya kuwekwa kwenye jokofu.

Kiasili, asali ilikuwa ikitumika kwa sababu maalum na kiasi kidogo tu, hivyo
hatari ya kumwongezea mtu uzito haikuwepo. Mara nyingi mtu anayetumia asali
alikuwa anatumia kijiko kimoja au viwili kwa siku na sio kila siku. Hata hivyo,
kumekuwa na imani potofu kwamba asali uweza kupunguza uzito wa mwili na
hivyo husababisha walengwa kutumia asali kwa wingi. Hii si kweli. Ikumbukwe
kwamba asali ina nishati-lishe kwa wingi ambayo huchangia kuongeza uzito wa
mwili hivyo huweza kuleta madhara iwapo itatumika kupita kiasi.

No comments:

Post a Comment

wasiliana nami