Monday, 29 September 2014

Athari za uzito ulio kithiri


Uzito uliozidi au unene uliokithiri una uhusiano mkubwa na
magonjwa sugu yasiyoambukizwa. Unene uliokithiri unachangia kwa kiwango
kikubwa kupata magonjwa sugu yasiyoambukizwa kama kisukari, magonjwa ya
moyo, shinikizo kubwa la damu na hata saratani. Unene unachangia katika kuzuia
mwili kutumia sukari kwa ufanisi; pia husababisha kuongezeka kwa mafuta
mwilini ambayo huweza kujikusanya kwenye mishipa ya damu na kufanya damu
isipite kwa urahisi hali ambayo husababisha msukumo mkubwa wa damu. Wakati
mwingine hali hii huweza kusababisha damu isifike kwa kiasi cha kutosha katika
viungo kama moyo, ubongo, misuli n.k. na kuweza kusababisha magonjwa ya
moyo kama moyo kushindwa kufanya kazi kabisa (heart failure) au moyo kukosa
damu ya kutosha (ischemic heart disease).

sababu za kupata uzito ulio kithiri.


Uzito wa mwili hutegemea kiasi na aina ya chakula unachokula
pamoja na shughuli unazofanya. Mara nyingi unene hutokana na kula chakula
kwa wingi kuliko mahitaji ya mwili na kutofanya mazoezi. Mahitaji ya chakula
mwilini hutegemea umri, jinsi; hali ya kifiziologia uliyonayo (kama una ujauzito
au unanyonyesha), kazi na mtindo wako wa maisha. Endapo kiasi cha chakula
unachokula kinatoa nishati – lishe kuliko mahitaji ya mwili, ziada hii huhifadhiwa

Thursday, 11 September 2014

Utafiti umeonyesha kuwa viwango vya gesi ya Carbon vimeongezeka duniani

Mkuu wa shirika la utabiri wa hali ya anga la Umoja wa Mataifa Michel Jarraud, ametoa tahadharti kuwa dunia nzima inapaswa kushughulikia mabadiliko ya hali ya anga haraka iwezekanavyo la sivyo muda unakwisha.
Takwimu mpya kutoka kwa shirika hilo, zinaonyesha kuwa viwango vipya vya gesi yenye sumu ya Carbon katika anga ya dunia viko juu zaidi.
Pia shirika hilo linasema kuwa kiwango cha gesi ya sumu ya Carbon Dioxide kinaendelea kuongezeka kwa kasi kuliko hali ilivyokuwa miaka mitatu iliyopita.
Shrika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO, linasema kuwa viwango vya gesi chafu viliongezeka kwa kasi zaidi tangu mwaka 1984.
Bwana Michel Jarraud alisema kuwa hapana shaka kwamba mabadiliko ya hali ya anga yanashuhudiwa na kwamba hali inaendelea kuwa mbaya zaidi.
Umoja wa mataifa unasema kuwa kuongezeka kwa gesi hizo kunasababisha mabadilko mabaya ya hali ya hewa hali ambayo inahitaji kuwe kauli moja ya mkataba wa dunia nzima kuweza kukabiliana na hali hiyo.

Ebola yatishia utaifa wa Liberia

Liberia inasemekana kuwa na changamoto za miundo mbinu kuweza kukabiliana na Ebola.
Liberia inakabiliwa na tisho kubwa kwa utaifa wake huku janga la Ebola likiendelea kuenea kwa kasi kubwa nchini humo.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa ya waziri wa ulinzi nchini humo.
Brownie Samukai aliambia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, kwamba juhudi za kimataifa za kupambana na ugonjwa huo hazina tija.
Shirika la afya duniani, limeonya kuwa maelefu ya visa vingine vya maambukizi huenda vikatokea nchini humo.

Athari za utumiaji wa chumvi kupita kiasi


Chumvi inapotumika kwa kiasi kidogo haina madhara. Miili yetu
huhitaji chumvi kwa kiasi kidogo sana. Kwa wastani tunahitaji
chini ya gramu 5 (kijiko cha chai) kwa siku. Hii Huupatia mwili madini ya
sodium yanayohitajika kwa siku. Lakini ni muhimu kukumbuka kwamba mwili
unapata pia madini haya kutoka kwenye vyakula vingine, hivyo chumvi itumike kwa kiasi kidogo. Kwa bahati mbaya tunatumia chumvi kupita kiasi. Matumizi ya chumvi nyingi yanaongeza uwezekano wa kupata shinikizo kubwa la damu,kwani chumvi husababisha maji kujikusanya mwilini. Maji yaliyojikusanya huongeza shinikizo kwenye moyo na mishipa ya damu na hivyo kusababisha moyo kufanya kazi

Faida za asali kiafya


Asali hutumika sio tu kama chakula bali baadhi ya watu huitumia
pia kama dawa. Asali ina uwezo wa kuondoa chembe chembe
haribifu mwilini na hivyo kuulinda mwili dhidi ya maradhi mbalimbali. Asali
ina virutubishi mbalimbali ikiwa ni pamoja na vitamini, madini na protini kwa
kiasi kidogo. Vilevile, asali ina sukari nyingi ambayo ni asilimia themanini (80%).
Kutokana na asali kuwa na sukari nyingi, asali ina nishati-lishe nyingi kama ilivyo

Saturday, 30 August 2014

Mawaziri wa Afya wajadili Ebola


Mtu akisoma tangazo kuhusu onyo dhidi ya maambukizo ya virusi vya ugonjwa wa Ebola mjini Monrovia, Liberia.
Mawaziri wa afya kutoka nchi za Afrika Magharibi wamekubaliana kuondoa upigaji marufuku wa safari za ndege na ufungaji wa mipaka kwa nchi ziliathirika kutokana na ugonjwa wa Ebola. Mawaziri hao ambao wamekutana mjini Accra, Ghana kupitia upya mikakati iliyokuwa ikitumika kupambana na virusi vya ebola

WHO:Hofu ya 20,000 kuambukizwa Ebola


Mawaziri wa afya wa Afrika Magharibi wanakutana Ghana kutafita njia za kupambana na Ebola
Shirika la afya duniani WHO limeonya kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola huko Afrika magharibi huenda ukasambaa na kuwaambukiza zaidi ya watu 20,000 kabla haujadhibitiwa.

Njia 5 za kuepuka virusi hatari vya Ebola


Njia za kuepuka kuambukizwa Ebola
Ebola:Njia tano za kujiepusha virusi hatari vya homa ya Ebola
Ebola ni mojawapo ya virusi hatari zaidi ulimwenguni lakini haiambukizwi kupitia hewa, hivyo basi huwezi kuambukizwa Ebola kama homa ya kawaida.
Madaktari wanasema kuepuka Ebola ni rahisi sana iwapo mtu atafuata tahadhari hizi muhimu zaidi:
1. Sabuni na maji
Nawa mikono kila baada ya shughuli yeyote kwa kutumia sabuni na maji safi- na utumie taulo kujikausha.
Hili huwa jambo gumu kwa wanaoishi kwenye

Ebola:Hofu yaendelea kutanda A.Magharibi


Liberia ni baadhi ya nchi zilizoathirika sana kutokana na Ebola
Kuna hofu kwamba mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, katika kanda ya Afrika Magharibi, utaendelea kuwa mbaya zaidi hadi kanda hiyo itakapopata afueni kutokana na ugonjwa huo.
Hii ni kwa mujibu wa maafisa wakuu wa afya nchini Marekani.
Mkurugenzi wa kituo cha udhibiti wa magonjwa , Tom Frieden,amesema kuwa ugonjwa huo unahitaji hatua zaidi ili kuweza kuudhibiti.

Ebola yaenea katika kitovu cha mafuta Nigeria


Kifo cha daktari huyo ni cha kwanza kutokea nje ya mji wa Lagos
Serikali ya Nigeria imethibitisha kutokea kifo cha daktari mmoja kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mji wa Port Harcout nje ya mji wa Lagos.
Watu wengine zaidi ya sabini wanachunguzwa mjini humo huku mke wa daktari huyo akiwekwa katika chumba chake kando kufanyiwa uchuguzi zaidi.
Daktari huyo alimtibu mgonjwa wa Ebola ambaye alifanikiwa kupona.

Mafuta yaliyo bora kwa afya


Mafuta ni muhimu mwilini, isipokuwa yanahitajika kwa kiasi
kidogo; hivyo kuepuka kabisa ulaji wa mafuta huweza kuleta
athari katika mwili, ikiwemo ubongo kutofanya kazi vizuri. Hata hivyo mafuta
yanapotumiwa kwa kiasi kikubwa yanaweza kuleta madhara mwilini. Hivyo ni
muhimu kuwa makini na kiasi cha mafuta kinacholiwa katika kila mlo.

Friday, 22 August 2014

Africa kusini yafunga Mipaka yake

Nchi ya Africa Kusini inafunga mipaka yake kwa wasafiri kutoka katika nchi za Liberia,Guine na Sierra Leone nchi hizo tatu zimeathiriwa vibaya na mripuko wa ugonjwa wa Ebola.

Waziri wa Afya wa taifa hilo, Aaron Motsoaledi,amesema kwamba marufuku hiyo haiwahusu raia wa nchi hiyo ingawa watalazimika kukaguliwa kitabibu ili kubaini endapo watakuwa wamepata

Thursday, 21 August 2014

Vitongoji hivyo vilivyoathirika na ugonjwa wa Ebola vya andamana huko Liberia


Maafisa wa usalama wakiwa Westpoint baada ya uvamizi wa kituo cha Ebola
Polisi nchini Liberia wamerusha vitoa machozi kuwatawanya umati uliojaa hasiria katika mji mkuu Monrovia wakipinga kuzingirwa kwa kitongoji chao na maafisa wa Usalama.
Maafisa wa usalama walilazimika kutumia nguvu baada ya waandamanaji kuanza kuwapura kwa mawe katika kitongoji cha Westpoint .

Wednesday, 20 August 2014

Serikali yatakiwa kupeleka vifaa vya kutambua ebola Tunduma

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Seleman Rashid.
Serikali imeombwa kupeleka haraka vifaa vyenye uwezo wa kuwatambua watu wenye maambukizi ya ugonjwa wa ebola katika mpaka wa Tanzania na Zambia mjini Tunduma ili kuepusha ugonjwa huo kuingia nchini kirahisi kwa kupitia katika mpaka huo.

Mpaka huo unatumiwa na nchi zaidi ya sita za Kusini mwa Afrika.

Ombi hilo lilitolewa na baadhi ya wakazi wa mji wa Tunduma kuhusiana na tahadhari inayoweza kuchukuliwa ili kuepusha ugonjwa huo ambao umeripotiwa kuenea katika nchi za Afrika Magharibi kuingia nchini.

Wananchi hao pia wameitaka serikali kuanza kutoa elimu kwa wananchi wanaoshi maeneo ya mipakani juu ya dalili za ugonjwa huo ili iwe rahisi kwao kujikinga na kutoa taarifa punde wanapomuona mtu mwenye dalili za kuugua ugonjwa huo.

Diwani wa Kata ya Tunduma, Frank Mwakajoka, alisema kuwa hadi sasa, hakuna elimu iliyotolewa kwa wananchi juu ya ugonjwa huo wala tahadhari iliyochukuliwa na serikali kwa wageni wanaoingia nchini kupitia mpaka wa Tunduma.

“Mpaka sasa hakuna jitihada zozote zilizofanywa na serikali kuwakinga Watanzania wasipatwe na maambukizi ya ebola kutoka kwa wageni wanaoingia nchini kupitia mpaka huu," alisema.

Naye Samwel Mkisi, mkazi wa Tunduma, alisema ugonjwa huo wanausikia tu kupitia kwenye vyombo vya habari.

Kaimu Ofisa Afya katika mpaka wa Tunduma, Jamal Mohamed, alisema kazi ya kuwapima wageni wanaoingia na kutoka ili kutambua kama wana maambukizi ya ebola, bado haijaanza kutokana na kutokuwapo kwa vifaa.

Hata hivyo, alisema kuwa tayari serikali imevituma vifaa hivyo kutoka Dar es Salaam na kwamba kazi ya upimaji itaanza mara moja.

Kwa upande wake, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mipakani mkoani Mbeya ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji, Lusarago Mleka, alisema kutokana na kutokuwapo kwa udhibiti wa kiafya, kunasababisha watumishi wa idara hiyo kufanya kazi kwa hofu.

Jinsi ya kuepuka magonjwa kirahisi

Adhari ya nyama zilizosindikwa
Nyama zilizosindikwa zimethibitishwa
kuongeza hatari ya kupata saratani hata
zikitumiwa kwa kiasi kidogo tu. Nyama
hizi zinahusishwa na saratani za kinywa,
koo, tezi la kiume (prostate), utumbo
mpana na mapafu. Inashauriwa kuepuka kutumia nyama zilizosindikwa. Nyama hizo ni pamoja na zile zilizosindikwa au kuhifadhiwa kwa chumvi, mafuta,kemikali au kukaushwa kwa moshi. Mfano wa nyama hizo ni soseji, nyama za kopo, hot-dog, salami, bacon.

Ebola:Wagonjwa 17 waliokuwa wametoroka katika kituo cha Monrovia wapatikana


Mmoja wa wanaume waliovamia kituo hicho na kumbeba mgonjwa
Waziri wa habari wa Liberia Lewis Brown amesema kuwa wagonjwa wote 17 wa Ebola waliokuwa wametoweka kutoka kwa kituo cha kuwatenga na umma wamepatikana.
Kupatikana kwao imekamilisha idadi ya wote 37 waliokuwa katika zahanati iliyovamiwa na wenyeji jumamosi iliyopita.
Wagonjwa 37 walikuwa katika kituo hicho cha Ebola kilichoko karibu na kitongoji cha WestPoint Viungani mwa

Monday, 18 August 2014

Albino akatwa kiungo Tabora

Matukio ya kukata viungo vya walemavu wa ngozi (albino), yameendelea mkoani hapa, ambapo juzi mlemavu wa pili katika muda usiozidi wiki mbili, amekatwa kiwiko cha mkono wake na wahusika kutoweka nacho kusikojulikana. soma zaidi

Waliokimbia zahanati ya ebola watafutwa


Ebola  Liberia
Kituo kilichotengwa na kuwekewa karantini kwa sababu ya ebola, kimeshambuliwa na zana kuporwa katika mji mkuu wa Liberia, Monrovia.
Watu kama 20 hadi 30 waliowekwa hapo kuangaliwa kama wana dalili za ebola walitoroka baada ya kituo hicho kuporwa Jumamosi usiku..

Sunday, 17 August 2014

Rais wa Colombia aunga mkono Bhangi



Rais wa Colombia aunga mkono kuhalalishwa kwa Bhangi
Rais wa Colombian Juan Manuel Santos amesema kuwa anaunga mkono matumizi ya bangi kwa minajili ya utabibu.
Bwana Santos ameunga mkono mswada ambao utapigiwa kura bungeni wakati wowote kwa manufaa ya kupunguza uchungu kwa wagonjwa .
Rais wa Colombia aunga mkono kuhalalishwa kwa Bhangi
Rais huyo amesema kuwa kuhalalishwa kwa Bangi kutawanyima walanguzi wa mihadarati biashara kwani itakuwa sio haramu kupatikana na bangi nchini humo.
Colombia ni moja kati ya mataifa ambayo yamekumbwa na vita vya walanguzi wa madawa ya kulevya na serikali vita ambavyo vimesababisha mauaji ya mamia ya watu. .
Marijuana inakuzwa kwa wingi nchini Colombia, lakini taifa hilo linajulikana kote duniani kwa ukuaji wa cocaine, kwa pamoja na Peru.
Bhangi inakuzwa kwa wingi nchini Colombia
Asilimia kubwa ya madawa hayo kulingana na takwimu yanauzwa nchini Marekani ambapo yanaingizwa kisirisiri kupitia mataifa ya Marekani ya kati na Mexico.
"natumai tutaliangazia jambo hili la matumizi ya marijuana kwa mtazamo mpya utakaofaidi wagonjwa ambao wanaitegemea kupunguza uchungu.'' alisema bwa Santos akiwa mjini Bogota